Ikiwa ni wiki 2 tu zimepita baada ya bibi aliyedhaniwa kuwa mchawi
(80) kukutwa nje ya nyumba ya mtu akiwa uchi hajitambui katika mtaa wa
Mageuzi kata ya Ndembeza mjini Shinyanga,matukio yanayohusishwa na imani
za kishirikina yameendelea kuacha watu midomo wazi ambapo leo asubuhi
binti anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 23- 25 aliyedaiwa kuwa mchawi
amekutwa hajitambui akiwa amevaa nguo nyeusi,kashikilia chungu kidogo
kwenye mlango wa nyumba ya mtu katika mtaa wa Bushushu kata ya Lubaga
katika manispaa ya Shinyanga huku akidai kuwa amefika mahali hapo kwa
kutumia chungu
Wakazi
wa Shinyanga wakiwa eneo la tukio nje ya nyumba aliponasa binti huyo
anayedhaniwa kuwa mchawi kutokana na nguo alizovaa na dawa nyeusi
alizopaka kwenye mwili wake.Binti huyo kwamba alifika mahali hapo na
wenzake kufanya sherehe baada ya kufanikisha uchawi wao wa kuharibu ndoa
ya Massawe aliyegoma kuoa ndugu yao na badala yake akaoa mwanamke
mwingine.


Mguu wa binti huyo aliyedai kutoka Ushirombo ukiwa umepakwa dawa nyeusi pamoja na usoni,mikononi na mgongoni.

Binti
huyo amesema leo ni mara ya tatu wanakuja kufanya uchawi wao,lengo lao
ni kutaka ndugu yao aolewe na Massawe,walikuja siku ya kwanza wakakuta
mke wa Massawe akisali,wakashindwa,wakarudi kwa mara ya pili kwa ajili
ya kusambaratisha ndoa,wakafanikiwa, leo yeye alikuwa kiongozi wa
wachawi wengine walikuja kufanya sherehe kwa kazi nzuri waliyoifanya
lakini wenzake wamemkimbia-

Wakazi wa Shinyanga wakichungulia kwenye madirisha kuona kinachoendelea ndani

ambapo
baada ya kumhoji binti huyo alisema alifika kwenye familia hiyo,akiwa
kiongozi wa kundi la wachawi zaidi ya 10 kutoka Ushirombo,Misungwi na
Shinyanga wakitumia vyungu na ungo majira ya saa 9 usiku kwa ajili ya
kufanya sherehe baada ya kufanikiwa kusambaratisha kichawi ndoa ya
Massawe na Mary Joseph.



Askari polisi wakimlinda Binti huyo asipigwe na wananchi waliofika eneo la tukio

Wananchi wakisubiri mchawi atoke ndani ya nyumba,,Aaskari polisi akimtoa ndani ya nyumba binti huyo ili kumpandisha kwenye gari la polisi

Binti akiondolewa eneo la tukio

Binti akiwa ndani ya gari la polisi



Wakazi wa Shinyanga wakiondoka eneo la tukio-
0 comments:
Post a Comment